Kipindupindu
ni miongoni mwa magonjwa ambayo husababishwa na aina ya bakteria aitwaye Vibrio cholerae, bacteria huyu
husababisha mtu kuhara majimaji yenye rangi kama maji ya mchele. Ugonjwa huu ni
wa kuambukizwa kwa njia ya viini vinavyoenezwa kupitia maji yaliyo changanyika
na kinyesi au matapishi kutoka kwa
wagonjwa wenye Kipindupindu. Mlundikano wa taka na maji machafu ni moingoni mwa
vyanzo vya maambukizi ya Kipindupindu.
Mlundikano wa Taka kwenye maeneo ya wapita njia
Aidha matumizi ya
choo yasiyo sahihi pia huchangia maambukizi ya ugonjwa huu. Kwa mujibu wa taarifa za ya idara ya huduma za
Afya na usafi wa mazingira Wizara ya Afya kipindupindu huenea kwa njia kuu
sita:
1:
kutokunawa mikono kwa maji safi na salama
yanayotiririka na sabuni kabla ya kula au baada ya kutoka chooni.
2:kula
chakula kilichoandaliwa katika mazingira yasiyo safi na salama.
3:
kunywa maji yasiyosafi na salama.
4:kumhudumia
mgonjwa mwenye dalili za kipindupindu bila kuzingatia kanuni za afya.
5:
usafirishaji holela wa wagonjwa wa kipindupindu.
6:
uandaaji na upikaji chakula bila kuzingatia kanuni za Afya.
Miongoni
mwa hatua za msingi katika kujikinga na maambukizi ya kipindupindu, ni kunawa mikono
wakati wowote kabla ya kutayarisha au kula chakula, kusafisha vyombo vya
chakula baada ya matumizi na kuvihifadhi sehemu safi. Ni muhimu sana kunawa
mikono kwa sabuni kwa utaratibu wa kuosha viganja, upande wa nyuma wa mkono,
katikati ya vidole na kucha na ufanye hivyo kwa sekunde chache baada ya kwenda
haja na kabla ya kula. Lingine ni kuwa na akiba ya maji yaliyochemshwa hususan pasipokuwa
na maji safi ya bomba.
Na Salim Gembe
Chanzo cha Habari:
Mtandao wa intaneti

No comments:
Post a Comment