Thursday, 1 October 2015

Chakula Bora

Unga wa dona kwa mchicha...

Kila Mtu anaweza kula chakula bora!
Ugali wa dona na mchicha ni maandalizi ya chakula cha bei nafuu mno…lakini ni miongoni mwa chakula bora.


Unga wa dona ulioandaliwa vizuri huwa una faida nyingi sana zaidi ya hata unga ambao umekobolewa. Faida hizo ni za kiuchumi au hata za kiafya. 

Faida ya Matumizi ya Unga wa dona

Kiuchumi:
1.      Ukisaga mahindi bila ya kukoboa unapata unga mwingi kwa kila kilo utakayoisaga. Hii ni kwa sababu ukoboaji wa mahindi kunapoteza kiasi fulani cha unga na virutubisho pia.
2.       Uandaaji wa mapishi ya unga wa dona ni rahisi zaidi katika ngazi ya familia.
Kiafya:
Katika Unga wa dona kuna kiasi kikubwa cha mafuta, protini, madini, vitamini, na nyuzinyuzi (fibre). Kwahiyo, unaimarisha zaidi lishe ya mlaji.

Faida za kula Mchicha(Kwa uchache)


1.      Huboresha mfumo wa Kinga mwili
2.     Huboresha uwezo wa kuona

3.     Huboresha mfumo wa akili na nevu (nervous system)

No comments:

Post a Comment

Matunda yanayo boresha mfumo wa KINGA YA MWILI

Katika kipindi hiki cha hofu ya corona ni muhimu sana kuhakikisha kinga yako ya mwili iko juu muda wote. Lakini pia ni vizuri katika maisha...