Saturday, 25 July 2015

Machungwa na zabibu hupunguza hatari ya kupata kiharusi

    Chuo cha Tiba cha Norwich huko Anglia Mashariki Uingereza, kimetafiti na kuangalia faida za matunda chachu (Citrus Fruit) pekee, kwa  mara ya kwanza tofauti na tafiti nyingi zinazo angalia umuhimu wa matunda na mboga za majani kwa afya kiujumla. Utafiti huu umehusisha maelfu ya wanawake lakini wataalamu wanaamini faida hizo za machungwa na zabibu pia zinapatikana kwa wanaume. Wataalamu hao wamechunguza umuhimu wa kemikali aina ya flavonoids ambayo ni jamii ya antioxidant (mada zinazoua kemikali hatari mwilini) inayopatikana katika matunda, mboga za majani na chokoleti nyeusi.


Utafiti huu uliochapishwa katika Jarida la Tiba la Kiharusi umesema kuwa, mada hiyo hupatikana kwa asilimia 82 kwenye machungwa na juisi ya machungwa, na hupatikana kwa asilimia 14 kwenye zabibu na juisi ya zabibu. Hata hivyo watafiti hao wamesema kwamba, kwa wale wenye kusudio la kuongeza kiwango kikubwa cha flavanones itawalazimu kula tunda asili la chungwa kwa wingi na si juisi za machungwa zinazotengenezwa kiwandani kutokana na kuwa na kiwango kikubwa cha sukari katika juisi hizo. Flavanones hutoa kinga dhidi ya kiharusi kutokana na kuongeza ufanisi wa mishipa ya damu kwenye ubongo na kutokana na kuwa na uwezo wa kuzuia maambukizi mwilini. 

 Lakini ni vyema tukawa makini pia kuwa matokeo ya utafiti huu yasiwafanye watu kuacha kula matunda ya aina nyingine pamoja na mboga za majani kwani nayo yana faida kubwa katika mwili wa binadamu. Pia tukumbuke kuwa, inawezekana kupunguza uwezekano wa kupata kiharusi kama mtu atakula lishe bora iliyo na virutubisho vyote muhimu, kula matunda na mboga za majani kwa wingi, kufanya mazoezi mara kwa mara, kupunguza kiwango chumvi tunachokula, (kwani watu wenye asili ya Afrika wana kiashiria cha asili kinachojulikana kama salt retention gene ambacho hufanya kiwango kidogo cha matumizi ya chumvi mwilini kionekane kikubwa na hivyo kuongeza hatari ya kupata kiharusi), kupunguza uzito, kupunguza kiwango cha matumizi ya mafuta katika chakula, kulala masaa ya  kutosha na kupunguza msongo wa mawazo.

Matunda yanayo boresha mfumo wa KINGA YA MWILI

Katika kipindi hiki cha hofu ya corona ni muhimu sana kuhakikisha kinga yako ya mwili iko juu muda wote. Lakini pia ni vizuri katika maisha...