Wednesday, 6 February 2019

UPUNGUFU WA DAMU MWILINI



 Upungufu wa damu mwilini ni hali ya mtu kuwa na upungufu wa haemoglobin kwenye mzunguko wa damu tofauti na kiwango maalum cha kitaalam kulingana na umri na jinsia ya mtu.
Upungufu wa damu mwilini unaweza kugundulika kwa kupima kiwango cha  seli hai nyekundu za damu , yani, hemoglobin na  haematicrit.
Kwa kawaida binadamu anatakiwa kuwa na kiwango maaluma cha damu Kama ifuatavyo :
                   UMRI/JINSIA
                KIWANGO CHA DAMU
Kabla ya kuzaliwa (cord blood)
 13.5- 20.5 (g/dl)
Siku moja baada ya kuzaliwa
15.0-23.5 (g/dl)
Miezi6  -  miaka 6
11.0 – 14.5 (g/dl)
Miaka 6 – miaka 14
12.0 -15.5 (g/dl)
Mtu mzima mwanamke
Mja mzito
12.0 – 15.0 (g/dl)
11.0 – 14.0 g/dl
Mtu mzima mwanaume
13.0 – 17.0 (g/dl)

Binadamu ana pokuwa na kiwango tofauti na hiyo au chini ya hivo huwa inamadhara kwake ,Inapotokea mtu akawa na upungufu hapo ana patiwa matibabu ya visababishi au kuongezewa damu.
sawa                                        Pungufu


                 VISABABISHI VYA UPUNGUFU WA DAMU MWILINI
Upungufu wa damu mwilini unaweza kusababishwa na vitu mbali mbali katika mazingira ya mwanadamu .Visababishi hivi kama;

ü  LISHE:hiki ni kisababishi kikuu katika kuchangia upungufu wa damu katika mwili                                                  wa binadamu. Hii hutokana na kukosa mlo kamili wenye virutubisho maalum katika kuboresha mzunguko wa damu mwilini,
ü  Mfano; vyakula vyenye madini ya chuma,folic acid, vitamin B,(nyama, mbogamboga,matunda),kukaa bila kula au kuto kulavizuri,ongezeko la uhitaji wa madini chuma mwilini,. Watu ambao hula kiasi kidogo cha vyakula vyenye madini chuma hukumbwa sana  na tatizohili.
ü  MAGONJWA:baadhi ya magonjwa huchangia pia   kwa kiasi kikubwa upungufu wa damu mwilini haswa magonjwa yale yanayo sambaa au kuenea kwa njia ya damu MFANO;tatizo  la figo ,ini,uvimbe au  tatizo kwenye mishipa ya damu,kama  hook worm , maambukizi ya                           muda mrefu pia husababisha mabadiliko au upungufu wa  damu mwilini,matatizo katika seli za damu au kinga za mwli, kutokana na damu nyingi nk.
ü  MAGONJWA YA KURITHI: kunabaadhi ya magonjwa  ya kurithi husababisha    mtu kuwa rahisikupatatatizo la upungufuwadamumwilini, kama vile watuwenyematatizokatikaselizadamu au vichochezivyauzalishajiwadamumwilini (haemoglobinopathies, G-6-P deficiency.nk)
ü   
TAKWIMU YA UPUNGUFU WA DAMU MWILINI:

 Takwim zinaonesha kuwa wanawake ndio wahanga wakubwa wa tatizohili la upungufu wa damu mwilini  ukilinganisha na wanaume . Pia madhara ya upungufu wa damu mwilini hutofautiana kulingana na sababu au visababishi MFANO; kutokwa au kupoteza damu nyingi (80%) hutegemeana na sababu na sehemu damu inayotoka, kupasuka mishipa ya damu 30-50%, vidonda vya tumbo 1%.


AINA ZA UPUNGUFU WA DAMU
·         Upungufu wa damu utokanao na lishe
·         Upungufuwa damu utokanao na mabadiliko ya mwili
·         Upungufu wa damu utokanao na magonjwa /maambukizi


DALILI ZA UPUNGUFU WA DAMU MWLINI
Mkono uliyo kwenye duara una upungufu wa damu


Watuwengi huwa na upungufu wa damu mwilini bila kuonesha dalili zozote .Dalili hujitokeza kulingana na kiwango cha upungufu wa damu na visababishi vyake.
Mtu mwenye upungufu wa damu mwilini huweza kuonesha dalilizifuatazo;

·         Kujihisi mchovu kupitakiasi bila kufanya shughuli yoyote
·         Maumivu ya viungo
·         Kushindwakuwa makini katika mambo yako (concentration)
·         Kupumua kwa nguvu au kwa tabu (kupumuaharaka au kubanwanapoumzi)
·         Hali inapokuwa mbaya zaidi mtu huweza kuonesha dalili za madhara kwenye moyo MFANO; mapigo ya moyo kwenda mbio sana, maumivu ya ghafla kwenye maeneoya moyo, kukaza na kuuma kwa misuli ya miguuni bila au baada ya kufanya shughuli.  Kukohoa sana,kupumua kwa shida,kutokw na jasho kupita kiasi,kutokwa na jasho kupita kiasi.
·         Dalili zinazo onekana ni kama kubadilika kwa rangi ya viganja na macho(vyeupe/njano), vidondamiguuni , kudhoofika na maumivu ya mifupa, kuvimba haswa miguuni.
            MADHARA YA UPUNGUFU WA DAMU MWILINI
·         Kushindwa kuvumilia mazingira ya baridi (cold intolerance)
·         Upungufu wa hewa safi (oxygen) kwenye viungo mbali mbali (kutokana na kiwango kidogo kinacho safirishwa kwenye damu)
·         Kwa mwanamke mjamzito ,hupelekea motto kutokukua vizuri tumbo ,kuzaa kabla ya mda(njiti) mtoto kufia tumboni ,chupa ya uzazi kupasuka kabla ya wakati.
JINSI YA KUJIKINGA NA TATIZO HILI.
·         Kula kwa wingi vyakula vyenye madini chuma. Kama vile dagaa nyama nk.
·         Kula vyakula vyenye protini kwa wingi kama vile mayai nyama maziwa nk.
·         Kula mboga mboga mf. Mchicha ,matembele na mboga zingine
·         Pia kula matunda kwa wingi nk.

N/B .Kuhakikisha kupata mlo kamili wenye virutubisho vyote, Nakujikinga na maambukizi ya magonjwa mbali mbali ambayo yanaweza kuwa kichochezi kwa tatizo hili.

No comments:

Post a Comment

Matunda yanayo boresha mfumo wa KINGA YA MWILI

Katika kipindi hiki cha hofu ya corona ni muhimu sana kuhakikisha kinga yako ya mwili iko juu muda wote. Lakini pia ni vizuri katika maisha...