Homa ya uzazi ni homa ambayo hutokea kwa mwanamke wiki sita baada ya kujifungua,hali hii
pia huweza kutokea kwa mwanamke alie jifungua kwa njia yoyote ya kawaida au upasuaji,pia hutokea wakati
wa kunyonyesha. Homa ya uzazi inaweza kuwa ni maambukizi kwenye sehemu ya maji
ya uzazi au maambukizi kwenye mji wa
mimba yani (endometritis) pia huweza kuwa ni homa yoyote baada au wakati wa
kujifungua. Visababishi vya Homa ya uzazi vinaweza kuwa kwasababu ya maambukizi
au wakati mwingine si kwa sababu ya maambukizi . Upande wa Maambukizi ambayo hutokea wakati wa kipindi
cha uzazi dalili zake kubwa ni homa lakini
jambo la kutiliwa maanani hapa ni kwamba sio kila homa inayotokea wakati wa
uzazi ni kwa sababu ya maambukizi, bali wakati mwengine huwa ni kawaida mzazi
kupata homa wakati wa uzazi.
Mwanamke anapopata
homa wakati wa uzazi, maranyingi huashiria maambukizi kwenye maji ya uzazi,maambukizi
kwenye mji wa mimda,maambukizi kwenye kidonda kwa wale waliozaa kwa njia ya
upasuaji,maambukizi kwenye matiti, maambukizi ya kwenye kidonda ukeni kwa wale
waliongezewa njia, maambukizi kwenye mfumo
wa upumuaji/hewa, mabaki ya uchafu tumboni maambukizi kwenye mfumo wa mkojo (UTI), pia matatizo ya upumuaji
yatokanayo na dawa za usingizi kwa wale walio jifungua kwa njia ya upasuaji.
Madhara yatokanayo na homa ya uzazi
Homa ya uzazi ni
moja ya sababu kubwa za magonjwa na vifo
kwa wakina mama walio jifingua hapa Tanzania. Kwa mujibu wa takwimu
zilizotolewa na wizara ya afya maendeleo
ya jamii, jinsia,wazee na watoto inakadiriwa kuwa asilimia 11% ya vifo vya
uzazi husababishwa na homa ya uzazi.Katika hali hii mama hufa kutokana na
maambukizi.
Visababishi vya homa ya uzazi
Homa ya uzazi inaweza kusababishwa kutokana na sababu
mbalimbali. Miongoni mwa sababu ambazo
husababisha homa ya uzazi ni pamoja na kufanya vipimo vya njia ya uzazi mara
nyingi isivyo kawaida,uchungu wa mda mrefu au kutofunguka kwa njia, chupa ya
uzazi kupasuka kabla ya wakati au kupasuliwa mapema, sababu nyingine ni kuzaa
kabla ya mda (miezi tisa) au kuzaa njiti,kuzaa kwa msaada wa kuongezewa njia au
kuzalishwa na vifaa vya kusaidia kuzalisha, kubakia kwa uchafu wa uzazi
tumboni, usafi wa mama binafsi,magonjwa
ya zinaa kwa mama,na upungufu wa damu wakati wa ujauzito.
Dalili atakazo onesha mama mwenye homa ya uzazi
Miongoni mwa dalili
za Mama mwenye homa ya uzazi ni pamoja na Joto la mwili kuwa juu kati ya
degiri thelathini na nane au zaidi, Maumivu ya tumbo la chini, Kutokwa
na uchafu wenye harufu mbaya ukeni, kondo la uzazi kuchelewa kupotea au kuwa na
maumivu, Majipu au kuvimba kwenye nyonga kutokwa na damu ukeni.
Jinsi ya kuzuia homa ya uzazi
Homa ya uzazi huweza
kuzuiwa kwa Kuzingatia usafi wakati wa kuzalisha na baada ya
kujifungua,kupunguza idadi ya vipimo vya njia ya uzazi kwa mama, kuzuia au kutokupasua
chupa ya uzazi mapema , Kupunguza muda wa uchungu kwa kutumia chati maalum au
mazoezi kwa mama, huduma maalum zitolewazo kwaajili ya uchungu ni muhimu, ni
muhimu pia mama kujitahidi usafi baada ya kujifungua.
By
Maunda Salim Gembe
Nuru ya siha project
Vyanzo vya habari:
-Baker,P.&Monga, A.(2006). Obstratrics by Ten Teachers
(18th ED). London: Hodder Arnold.
-Oats, .J., Abraham, S.(2005) Llewellyn-Jones Fundamental of
Obstetrics and Gynaecology. (8th Ed).Edinburgh:Mosby.
-DeCherney,A.H.&Nathan,L.(2002)Current Obstetrics and
Gynaecology (9th Ed).McGraw Hill.
ACCESS MEDICAL & DIALYSIS CENTER
H.H MUSSA
0715 620245

