Thursday, 20 August 2015

vyakula vinavyoimarisha afya ya ngozi

 Kula chakula chenye virutubisho sahihi ni jukumu la lazima la binadamu ili kuwa na afya njema. Dunia ina vyakula vya asili ambavyo ndani yake kuna virutubisho muhimu vinavyosaidia mwili kupambana na magonjwa na pia kuimarisha afya. Vyakula hivyo ni vile vya kijani ambavyo vina uwezo mkubwa zaidi katika kuponya magonjwa na kusaidia pia kukarabati, kujenga mwili na kuimarisha siha.                       
 Ngozi nayo ni sehemu muhimu ya mwili ambayo ina jukumu kubwa la kuukinga na kuufunika mwili na viungo mbalimbali na afya yake ni jambo la kuzingatiwa. Aina za vyakula tunavyopendelea kula vinaweza kuchangia katika muonekano wa ngozi zetu.
 Kuna aina za vyakula vinavyosaidia katika kutunza ngozi yako bila gharama kubwa. Bi Samatha Heller mtaalamu wa lishe katika Chuo Kikuu cha Tiba cha New York City anasema kuwa, kila tunachokula kinakuwa sehemu ya mwili wetu na kila tunapo vyakula bora ndivyo ngozi zinavyoonekana vizuri. Naye Elein Linker mtaalamu wa biokemikali na mwasisi wa kituo cha kutunza ngozi cha DDF anasema, matatizo mengi ya ngozi kama vile chunusi ya aczema (ngozi kuwa nyekundu,kuvimba,kuwasha au ukavu) itching and dryness  yanaweza kuwa yanahusiana na lishe. Hivyo tunashauriwa kujitahidi kufuata kanuni za afya ili kuufanya mwili uwe na afya nzuri kwa kula chakula bora, kufanya mazoezi, kupumzika kwa muda mrefu, vivyo hivyo ngozi nayo inatakiwa kutunzwa vyema kupitia lishe.


  Asali ambayo hutengenezwa na nyuki kwa viambato asilia ni chakula muhimu kwa ajili ya kuimarisha afya ya ngozi na pia afya ya binadamu. Sababu kubwa ya kutumia mafuta ya kuipaka ni kuifanya ngozi iwe na unyevu nyevu. Asali husaidia kutunza na kuhifadhi unyevu kwenye ngozi na ina kiwango kikubwa cha sukari na asidi ambazo huzuia vijidudu wanaozaliana kwenye ngozi. Vyakula vingi vya baharini pia vina kiwango kikubwa cha Zinc na Omega 3 ambazo ni muhimu kwa siha ya ngozi. Faida za Omega 3 ni pamoja na kuondoa kukakamaa au ukavu wa ngozi, kupunguza kuvimba na kukunjamana kwa ngozi na husaidia mzunguko mzuri wa damu mwilini hivyo kuboresha ngozi.
 Kiini cha yai kina vitamini A na B huku sehemu yenye ute ikiwa na protini nyingi ambayo ni muhimu pia kwa ngozi . Mada ya Tretinoin inayopatikana kwenye Vitamin A husaidia kuondoa chunusi na mikunjo ya ngozi. Mada nyingine ya Biotin inayopatikana kwenye Vitamin B ni muhimu kwa afya ya ngozi na kucha na protini inayopatikana kwenye ute wa yai ni muhimu katika kuifanya ngozi iwe nyororo na yenye kung'aa na pia husaidia ngozi kujilinda vizuri na mionzi ya jua.



 Matunda yenye vitamini C kama vile chungwa, limao na mengineyo ni muhimu pia katika kuimarisha afya ya ngozi, kwa sababu husaida kutengeneza collagen, ambayo ni aina ya protini inayotengeneza ngozi. Vitamini C inasaidia kuondoa uvimbe na mikunjo ya ngozi na hivyo kuilinda ngozi isizeeke mapema.
Mboga za majani pia ni muhimu kwa afya ya ngozi kama tujuavyo zimesheheni vitamin na virutubisho vya aina mbalimbali vyenye faida kubwa kwa ngozi na mwili kwa ujumla.

Chanzo cha habari: Mitandao 

No comments:

Post a Comment

Matunda yanayo boresha mfumo wa KINGA YA MWILI

Katika kipindi hiki cha hofu ya corona ni muhimu sana kuhakikisha kinga yako ya mwili iko juu muda wote. Lakini pia ni vizuri katika maisha...