Wednesday, 19 August 2015

Ugonjwa wa Kipindupindu

  Kipindupindu ni miongoni mwa magonjwa ambayo husababishwa na aina ya bakteria aitwaye Vibrio cholerae, bacteria huyu husababisha mtu kuhara majimaji yenye rangi kama maji ya kupikia mchele. Ugonjwa huu ni wa kuambukizwa kwa njia ya viini vinavyoenezwa kupitia kwa kinyesi kutoka kwa wagonjwa wenye Kipindupindu.Mlundikano wa taka na maji ma chafu  pia ni moingoni mwa vyanzo vya Kipindupindu.


                                                                                                   
Mlundikano wa uchafu ndiyo chanzo cha Kipindupindu
Miongoni mwa hatua za msingi katika kujikinga na maambukizi ya kipindu pindu ni kunawa mikono wakati wowote kabla ya kutayarisha au kula chakula, kusafisha vyombo kama sahani, vikombe n.k. Nawa mikono kabisa kwa sabuni – kiganja, upande wa nyuma wa mkono, katikati ya vidole na kucha kwa sekunde baada ya kwenda haja na kabla ya kula na kuwa na akiba ya maji yaliyochemshwa pasipo na maji safi ya bomba.
Chanzo cha Habari: Mtandao wa intaneti

No comments:

Post a Comment

Matunda yanayo boresha mfumo wa KINGA YA MWILI

Katika kipindi hiki cha hofu ya corona ni muhimu sana kuhakikisha kinga yako ya mwili iko juu muda wote. Lakini pia ni vizuri katika maisha...